Posts

Showing posts from November, 2024

Takukuru Kagera kuchukua hatua dhidi ya Rushwa kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa.

  Na Lydia Lugakila Bukoba Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Kagera imesema haitasita kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wale wote watakaojihusisha na vitendo vya Rushwa kabla ya uchaguzi wa Serikali za mitaa,wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi. Kauli hiyo ya imetolewa na Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Kagera Ezekia Sinkara wakati akiongea na waandishi wa Habari katika ukumbi wa Taasisi hiyo uliopo Manispaa ya Bukoba ikiwa ni katika utekelezaji wa majukumu ya Taasisi hiyo katika kipindi cha Julai hadi Septemba 2024. Sinkala amesema kuwa wamejipanga vizuri kuhakikisha wanaendelea kutoa kutoa elimu kwa Wananchi pamoja na makundi mbali mbali ikiwemo viongozi wa Kisiasa kwa lengo la kuhakikisha uchaguzi unafanyika bila kuwepo vitendo vya Rushwa . " Sote tunatambua tunaelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa Novemba 27,2024 ambapo kwa sasa shughuli mbali mbali za mchakato huo zinaendelea hivyo hatutaki kuona wala kusikia wanaojihusisha na vitendo vya Rushwa...

Wanakijiji Karagwe Kunufaika na Kivuko cha Kisasa Ziwa Burigi

  Na Lydia Lugakila Karagwe Wananchi katika kata za Rugu na Nyakasimbi, pamoja na maeneo jirani katika wilaya ya Karagwe Mkoani Kagera wanatarajia kuondokana  na adha ya kuvuka Ziwa Burigi kwa mitumbwi isiyo salama.  Serikali, kupitia Wizara ya Ujenzi, imetangaza mipango ya kuleta kivuko cha kisasa kitakachorahisisha usafiri na kuboresha usalama wa wakazi wa maeneo hayo. Hayo yamebainika katika kikao cha Baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe kilichofanyika katika ukumbi wa Angaza  Novemba 13,2024. Waziri wa Ujenzi na Mbunge wa Jimbo la Karagwe, Innosent Bashungwa, ametangaza habari hiyo njema kwa wananchi. “Kwa muda mrefu wananchi wa kata hizi wamekuwa wakitumia mitumbwi kuvuka ziwa hili ili kufanya shughuli zao za maendeleo" alisema Waziri Bashungwa. Waziri Bashungwa alisema, Serikali imeona umuhimu wa kuleta kivuko cha kisasa ambacho kitahakikisha usalama na kurahisisha shughuli zao. Kuvuka kwa mitumbwi kumeonekana kuwa hatarishi, ambapo Wananchi w...